Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Mwili wa Mwanafunzi Wakutwa Ndani ya Nyumba

Taharuki na sintofahamu imetanda katika Mtaa wa Igodima jijini Mbeya baada ya mkazi wa eneo hilo anayedaiwa kuwa mwalimu na mwanafunzi wa Chuo Kikuu, Zainabu Mwalyepelo, kukutwa amefariki dunia nyumbani kwake.

Taharuki hiyo imetokea leo Alhamisi Januari 15, 2026 katika eneo hilo baada ya baba mzazi wa marehemu, Jacob Mwalyepelo kufika nyumbani hapo na uongozi wa serikali ya mtaa huo kubomoa mlango na kukuta mwili kwenye sofa.

Akizungumza huku akitokwa machozi, Mwalyepelo amesema ni maumivu makali kumpoteza mtoto wake ambaye amehangaika naye kwa muda mrefu na gharama kubwa kwa matibabu.

Amesema mwanaye alikuwa mwalimu kitaaluma na alikuwa akijiendeleza kielimu katika Chuo Kikuu cha Catholic Mbeya (CUoM).

"Naumia jamani, bora ningekufa mimi niliyezeeka, nimehangaika sana na mwanangu kuanzia India, Hospitali ya Rufaa Kanda, leo mtoto wangu anakufa, nifanyeje," amesema.

Akimzungumzia mdogo wake, kaka wa marehemu, Christopher Mwalyepelo amesema mdogo wake hakuwa na mume wala mtoto na alikuwa akisumbuliwa na tatizo la moyo na wakati mwingine kubanwa na kifua.

Amesema kwa muda ambao alitoka hospitali hakupenda kukaa sehemu ya kelele, hali iliyomfanya kuwa mwenyewe nyumbani kwake katika mtaa huo.

 

 

 

Chanzo; Mwananchi

Kuhusiana na mada hii: