Wanawake wa Kata ya Iganzo jijini Mbeya, wamelalamika kubakwa na vijana wadogo ambao ni madereva wa Bajaji wa Kijiwe cha Kibaoni na kwa mama bunju, wakidai kuporwa mali zao, kutekwa na kwenda kutupwa maporini, pindi wanapotoka kwenye shughuli zao za kiuchumi hali iliyozua hofu ya usalama wa maisha yao.
Baada ya kukithiri kwa matukio ya uvunjaji wa sheria ikiwemo uvutaji bangi,uchezaji kamari, ulevi muda wa kazi ubakaji na wizi, uongozi wa Kata ukalazimika kuita mkutano wa hadhara, ili kuwataja hadharani wanaodaiwa kufanya vitendo hivo.
Chanzo; Itv