Wakati baadhi ya wateja wakilalama kuhusu kuisha haraka kwa umeme wanaonunua kupitia mfumo wa Luku, Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), limesema hakuna jibu la moja kwa moja bila kufanyika tathmini ya kitaalamu.
Kwa mujibu wa waliotoa malalamiko, wamekuwa wakinunua umeme kiwango kilekile lakini huisha ndani ya muda mfupi licha ya kuwa hawajaongeza matumizi ya nishati hiyo.
Akizungumza na Mwananchi Januari 23, 2026 Mkurugenzi wa Tanesco, Lazaro Twange, amesema hakuna jibu la moja kwa moja linaloweza kutolewa bila kufanya tathmini ya kitaalamu katika eneo husika.
Chanzo; Mwananchi