Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Polisi Wakanusha Kuzuia Wananchi Kula Mchana Ramadhan, Zanzibar

Jeshi la Polisi, Kamisheni ya Polisi Zanzibar, limekanusha vikali taarifa zinazosambazwa katika mitandao ya kijamii zikidai kuwa limetoa tamko la kuzuia wananchi kula mchana katika mwezi Mtukufu wa Ramadhani, likieleza kuwa taarifa hizo si za kweli na hazijatolewa na Jeshi hilo.

Kupitia taarifa yake rasmi ya Kamishna wa Polisi Zanzibar CP Kombo Khamis Kombo, imeeleza kuwa uvumi huo hauna msingi wowote na umelenga kupotosha umma, hivyo limewataka wananchi kupuuza taarifa hizo na kuendelea na shughuli zao kama kawaida.

Aidha, Jeshi hilo limewasihi wananchi kuendelea kudumisha amani na utulivu pamoja na kuheshimu mila, desturi na sheria za nchi katika kipindi chote cha mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Jeshi la Polisi pia limekumbusha umuhimu wa kupata taarifa sahihi kupitia vyanzo rasmi vya Jeshi hilo na kuepuka kusambaza taarifa zisizo na uthibitisho, ambazo zinaweza kusababisha taharuki au upotoshaji katika jamii.

 

 

Chanzo; Wasafi Media

Kuhusiana na mada hii: