Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Baba, Mama na Mtoto Wafariki kwa Moto Kigoma

Familia ya watu watatu, akiwemo baba, mama, na mtoto wa miaka mitatu katika Kata ya Kagera, Manispaa ya Kigoma Ujiji, wamefariki dunia baada ya nyumba yao kuchomwa moto mara baada ya kumwagiwa petroli usiku wa kuamkia Januari 25, 2026.

Chanzo cha tukio hilo la kinyama kinadaiwa kuwa ni mgogoro wa mirathi unaohusisha ugomvi wa mali za wazazi ndani ya familia hiyo.

Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, Dkt. Rashid Chuachua, amethibitisha kutokea kwa mkasa huo akiwa katika eneo la tukio, ambapo ameeleza kuwa watu hao walikutwa wamefariki dunia baada ya nyumba yao kuteketea kabisa.

Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi ili kubaini waliohusika na shambulio hilo la kikatili.

 

 

Chanzo; Mwananchi

Kuhusiana na mada hii: