Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Marehemu Kuzikwa Ndani ya Nyumba Isiuzwe

Familia ya kijana Elia Msuya aliyefariki akiwa anapatiwa matibabu baada ya kudaiwa kupigwa jiwe kisogoni na mwenzake wakiwa kwenye ugomvi ambaye alikuwa ni mkazi wa kata ya Murieti Mkoani Arusha imeamua kuvunja sehemu ya nyumba yake ili azikwe baada ya kutokea kwa ugomvi ambao inaelezwa kuwa ndugu walitaka kuuza eneo hilo

Israeli Msuya msemaji wa familia hiyo amesema kwamba eneo hilo ni dogo na baadhi ya ndugu walitaka liuzwe ili wakalipe gharama za hospitali lakini kama familia wamekaa na kukubaliana kuwa eneo hilo halitauzwa bali litaachwa ili mke na watoto wa marehemu waishi hapo

Kwa upande wa dada wa marehemu ameomba serikali iweze kuwasaidia deni la shilingi million moja na laki tano wanalodaiwa hospitalini kwa kuwa familia haina uwezo

 

Chanzo; Millard Ayo

Kuhusiana na mada hii: