Katika hali isiyokuwa ya kawaida, familia ya Daniel Peter Wakazi wa Kata Malangarini, Wilaya ya Arumeru Mkoani Arusha inayoomboleza msiba wa Ndugu yao, imejikuta ikipata maumivu juu ya maumivu baada ya Wezi kuingia ndani ya nyumba yao kwa kupita kwenye paa na kuiba vitu mbalimbali ikiwemo pikipiki na simu baada ya Wafiwa kupatwa na usingizi mzito.
Edna Samson mmoja wa Wanafamilia hao, amesema siku ya tukio walilala saa tisa usiku ambapo baada ya kulala walipitiwa na usingizi mzito ambao ulifanya wasisikie chochote kikiibwa ambapo ameongeza kuwa waliporipoti tukio hilo Polisi na Watuhumiwa kupatikana lakini baadae wakaachiwa.
Edna na Familia yake wameziomba Mamlaka ziendelee na uchunguzi zaidi na hatua kali za kisheria zichukuliwe dhidi ya Wahusika wote, juhudi za AyoTV kupata taarifa kuhusu wizi huu kutoka kwa Kamanda wa Polisi Arusha bado zinaendelea.
Chanzo; Millard Ayo