Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Kesi Ya Lissu Yafikishwa kwa Rais Samia

Wakili Boniface  Mwabukusi, Rais wa Chama cha Wanasheria cha Tanganyika “TLS” ameoridhesha hoja za msingi walizowasilisha kwa Rais wa Jamhuri wa Tanzania, kupitia kipindi cha 360 cha Clouds Tv.

"Hoja za msingi tulizozungumza na Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ni suala la sheria na kanuni za tume za uchaguzi kwanini zinalalamikiwa na maeneo yanayolalamikiwa.

"Na jambo la pili tulilowasilisha kwake ni suala la umuhimu wa kuwepo kwa mazungumzo au mjadala wa Kitaifa kabla na baada ya uchaguzi ili kulileta Taifa pamoja. Na sisi kuona namna gani tunapita kwenye hii changamoto salama.

"Na jambo la Tatu ni shauri la Mhe. Tundu Lissu linaloendelea mahakamani na mtazamo wetu kidemokrasia na Kimataifa kwa Taifa letu na kuomba waone kitu gani kama Serikali watafanya. Na kwamba shauri la Tundu Lissu watu wanaliangalia kwa sura tofauti na halileti taswira nzuri kwa Taifa letu"- Mwabukusi

 

Chanzo: Clouds Tv

Kuhusiana na mada hii: