Jeshi la Polisi Mkoa wa Kigoma linafanya uchunguzi, juu ya taarifa ya kutoweka kwa Mahamoud Juma Abdallah (25), mkazi wa Mtaa wa Mwasenga, manispaa ya Kigoma Ujiji, Mfanyabiashara katika Soko la Buzebazeba, ambaye inasemekana allichukuliwa na watu wasiofahamika, tukio ambalo liliripotiwa Februari 19 saa tatu asubuhi.
Taarifa ya Jeshi la Polisi iliyosainiwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, inawasihi wananchi kuwa watulivu wakati uchunguzi ukiendelea, ili kubaini ukweli wa tuhuma hizo na kuwachukulia hatua wahusika watakapobainika.
Chanzo; Itv