Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema amesikia sauti za Vijana na amewahakikishia kuwa soko la Jangwani litajengwa pale utakapokamilika ujenzi wa daraja la Jangwani.
Rais Samia amesema hayo leo February 08,2026 wakati akizindua soko la Kariakoo.
“Na leo hapa niliambiwa kuna Wanangu Wamachinga ambao walitaka kuingia na fulana zao waniambie Mama tunasubiri soko la kule Jangwani lakini mmewazuia kuingia nataka niwaambie Wanangu sauti zenu nimezisikia na soko lile tupo katika hatua ya kulijenga”
“Kuna mambo yanafanyika tuweke bonde sawa tujenge soko, Serikali ipo tayari kujenga soko tukishajenga daraja, sauti zenu nimezisikia soko tutalijenga Jangwani”
Chanzo; Millard Ayo