Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Lema Adakwa Arusha

Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Godbless Lema anadaiwa kukamatwa Jijini Arusha na jeshi la polisi ikiwa ni siku moja tangu jeshi hilo kutoa wito kwa baadhi ya viongozi wa chama hicho kujisalimisha kwa jeshi hilo kwa tuhuma zinazohusiana na vurugu na maandamano wakati wa Uchaguzi Mkuu Oktoba 29.

Taarifa ya kukamatwa kwa kiongozi huyo imetolewa na Katibu wa CHADEMA Kanda ya Kaskazini, Ndonde Totinan ambaye ameeleza kuwa Lema amekamatwa eneo la Usa River mkoani Arusha.

Katika orodha ya viongozi wa CHADEMA wanaotakiwa kujisalimisha polisi kwa mujibu wa taarifa ya jeshi hilo ya Novemba 7, mbali na Lema yumo John Mnyika, Deogratius Mahinyila, Hilda Newton, Brenda Rupia, Award Kalonga, Boniface Jacob, Amani Golugwa na Machumu Kadutu.

 

Chanzo; Nipashe

Kuhusiana na mada hii: