Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Tatizo Adaiwa Kumuua Mama Yake wa Kambo Kisa Mashamba

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia Tatizo Yohana Mzumbwe, mkazi wa Masoko mkoani Mbeya kwa tuhuma za mauaji ya mama yake wa kambo, Merry Yohana kwa kumkata na panga kichwani.

Taarifa ya kamanda wa Polisi mkoa wa mbeya Kamishna msaidizi mwandamizi wa polisi Benjamini Kuzaga inaeleza kwamba mtuhumiwa anadaiwa kutenda tukio hilo Oktoba 6,Kijiji cha Mapinduzi, Kata ya Masoko, Mkoani Mbeya, kwa kumuua mama huyo ambaye alikuwa mwenye ualbino na na kukimbia.

Kuzaga amesema Uchunguzi wa awali umebaini kuwa chanzo cha tukio hilo ni mgogoro wa kifamilia kuhusu mashamba ambapo mtuhumiwa alikuwa akimshinikiza Marehemu kugawa mashamba ya urithi yaliyoachwa baada ya baba yake kufariki.

 

Chanzo: Wasafi

Kuhusiana na mada hii: