Fainali za mashindano ya Utafiti ya CFA (CFA Research Challenge) ambayo huwakutanisha Wanafunzi wa Vyuo Vikuu vya Afrika Mashariki ikijumuisha nchi za Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda pamoja na Ethiopia zimefanyika ambapo Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UDSM) kimeibuka mshindi kwa mwaka huu 2026.
Mashindao hayo ambayo yamedhaminiwa na Benki Kuu ya Tanzania (BOT), CMSA, DSE Exodus Advisory, Intrust Tanzania pamoja na Benki ya NMB huwapa nafasi Wanafunzi wanaosoma Masomo ya biasha, uchumi na uwekezaji kushiriki na kujifunza kwa nadharia na kwa vitendo namna ya uendeshaji wa Soko la Hisa (DSE), Soko la Mitaji (CSMA) ambapo rasilimali watu hujitolea kuwafundisha na kiwasimamia wanafunzi walioshiriki katika utafiti huo kwa kipind kisichopungua miezi sita na kisha huanda ripoti ambayo hushindanishwa katika mashindano hayo.
Chanzo; Millard Ayo