Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Viongozi wa Chadema Waachiwa kwa Dhamana

Viongozi kadhaa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) waliokuwa wameshikiliwa na Jeshi la Polisi wakiongozwa na Makamu Mwenyekiti, John Heche wameachiwa huru kwa dhamana hii leo Novemba 10, 2025.

Taarifa zilizotufikia zinaeleza kuwa, viongozi hao waliokuwa wakishikiliwa vituo mbalimbali vya Polisi nchini wameachia katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay jijini Dar.

Mbali na Heche, wengine walioachiwa huru ni Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho upande wa Bara, Amani Golugwa, Mwenyekiti wa Kanda ya Pwani, Boniface Jacob au Boni Yai na Mjumbe wa Kamati Kuu, Godbless Lema.

 

Chanzo; Global Publishers

Kuhusiana na mada hii: