Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Mtoto wa Miaka 15 Atoroka Nyumbani Adai Anaenda Kutafuta

Mtoto Daniel Jeremiah (15) Mkazi wa Kata ya Olorieni, Wilaya ya Arumeru Mkoani Arusha ameripotiwa kutoroka nyumbani kwao anapoishi Mama yake na kumuachia ujumbe ya kuwa anakwenda kujitafuta na kwamba anamuonea Mama yake huruma jinsi anavyomuhangaikia.

Ujumbe huo umesomeka “Mama samahani lakini mimi nimeamua kuondoka naona hii ndio njia peke itakayokufanya usihangaike kunitafutia hela mimi ngoja niondoke nikajitafute wewe kaa mwenyewe, sio kwa ubaya Mama ninakuonea huruma unavyonihangaikia mimi, naomba unisamehe kama nimekosea".

Akizungumza na Ayo Tv, Jackline ambaye ni Mama Mzazi wa Daniael amesema wamekuwa wakiishi vizuri na Mtoto wake kama Marafiki na kwamba hajawahi kumsimulia changamoto yoyote ya maisha ambapo amekuwa akimuhudumia kwa kumpatia mahitaji yote ya muhimu kama Mzazi.

 

Chanzo; Millard Ayo

Kuhusiana na mada hii: