Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Wanafamilia wa Tano Wafariki Dunia Wakitoka Mazikoni

Wanafamilia watano wa familia ya Francis Kaggi, wamefariki dunia baada ya kupata ajali, wakitoka kwenye maziko mkoani Tanga.

Taarifa iliyosambazwa miyandaoni huku ikionesha wanafamilia hao, pamoja na ratiba ya mazishi, imewataja walifariki kuwa ni Francis Kaggi, na wanawe waanne Janemary Kaggi, Maria Kaggi, Joshua Kaggi, Elineema Kaggi.

Imeeleza kwamba, Mtoto wake wa pili alitarajia kuanza elimu yake ya juu Chuo Kikuu Ardhi (ARU), na wa kwanza wa kike alikuwa anafanya kazi mkoani Tabora na mdogo alikuwa anasoma shule ya awali. Na mwingine alikuwa anafanya kazi Tanesco.

Chanzo cha vifo ni ajali, wakitoka kumzika mama wa mumewe siku ya Alhamisi, na Jumapili walianza safari asubuhi, huku mume ambaye ni Francis, akiwa ni dereva wa gari hilo.

Inaelezwa mkewe Francis, pekee amenusurika ajalini, na dada wa kazi akiwa amelazwa chumba cha uangalizi maalum (ICU).

 

Chanzo; Nipashe

Kuhusiana na mada hii: