Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Rais Samia Amuapisha Dr Mwigulu Kuwa Waziri Mkuu

Baada ya uteuzi, kisha kuidhinishwa na bunge, hatimaye Dk Mwigulu Nchemba ameapishwa rasmi kushika wadhifa wa Waziri Mkuu wa Tanzania.

Mbunge huyo wa Iramba Mashariki, ameapishwa leo Ijumaa Novemba 14, 2025 Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma, mbele ya Rais Samia Suluhu Hassan.

Hatua ya kuapishwa kwake, inafungua rasmi milango ya kuanza utekelezaji wa majukumu ya mtendaji mkuu wa Serikali ya awamu ya sita kipindi cha pili.

Dk Mwigulu anashika nafasi hiyo kumrithi, Kassim Majaliwa aliyeongoza kwa miaka 10 tangu mwaka 2015.

 

Chanzo; Mwananchi

Kuhusiana na mada hii: