Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Watatu Jela Miaka 20 kwa Kukutwa na Silaha

Mahakama ya Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi imewahukumu kifungo cha miaka ishirini jela Mashili Ndaki (48) Mayekra Kamwina (44) na Mayela Richard (38) wote wakazi wa Kaliua Mkoani Tabora baada ya kupatikana na hatia ya kukutwa na silaha mbili haramu aina ya gobore na vipande nane vya nyama ya kiboko.

Hukumu hiyo imetolewa Februari 11, 2026 na Hakimu wa Mahakama hiyo Mhe. Fahamu Kibona.

Awali imeelezwa Mahakamani hapo kuwa washtakiwa hao walitenda kosa hilo April 24, 2025 huko Sense ndani ya pori la akiba ugala.

Watuhumiwa hao walifikishwa Mahakamani hapo kwa mara ya kwanza Mei 23, 2025 na shauri hilo kusajiliwa kesi ya uhujumu uchumi namba 8375 ya mwaka 2025

Kesi hiyo ilikuwa na jumla ya mashahidi 5 ambapo mahakama hiyo imeeleza kuwa imeridhishwa na ushahidi uliotolewa pasi na shaka uliotosha kuwatia hatia watuhumiwa.

 

 

Chanzo; Bongo 5

Kuhusiana na mada hii: