Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Msimamo wa Urusi Kubadilika Sababu Shambulio la Droni Nyumbani ya Rais

Rais wa Urusi Vladimir Putin alimwambia Rais wa Marekani Donald Trump kwamba Urusi itaupitia upya msimamo wake kuhusu mazungumzo ya amani baada ya kile ambacho Moscow imedai ni shambulio la droni la Ukraine kwenye makazi ya rais wa Urusi.

“Msimo wa Urusi Utabadilika baada ya shambulio la droni la Ukraine kwenye makazi ya Rais.” - Putin

Ukraine imepinga madai ya Urusi kwamba droni 91 zilishambulia makazi ya Putin kaskazini mwa Urusi, ikiyaita uongo, na imeishtaki Moscow kwa kujaribu kudhoofisha mazungumzo ya amani.

 Mshauri wa sera za kigeni wa Kremlin, Yuri Ushakov, alisema kwamba Putin na Trump walizungumza Jumatatu na kwamba Putin alipewa taarifa na Trump pamoja na washauri wake wakuu kuhusu mazungumzo na Ukraine.

 Putin alimjulisha Trump kuhusu shambulio la droni kwenye makazi ya rais wa Urusi na akamwambia Trump kwamba Urusi inapitia upya msimamo wake kutokana na tukio hilo.

 

Chanzo; Dw

Kuhusiana na mada hii: