Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Waziri Mkuu Aibuka wa Wanaofungua Kampuni za Kigeni na Kujifanya Wazawa

Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mwigulu Nchemba, amewaonya Watu wanaoanzisha Kampuni na kuziita ni Kampuni za Wazawa wakati kiuhalisia zinamilikiwa na Wageni.

Dkt. Nchemba ameyasema hayo hii leo Februari 16, 2026 akikagua mradi wa bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima, Uganda hadi Chongoleani, Tanga ikiwa ni sehemu ya ziara ya Kiserikali Mkoani humo.

“Wapo wasio waaminifu wanawatumia Watanzania kuanzisha Makampuni wanasema ni ya wazawa, tunataka kuinua Kampuni za Watanzania, upo mchezo Mgeni anatumia anuani ya Mtanzania ambaye si mnufaika, wale watakaogundulika wanafanya ujanja tutawafungia na hawatafanya kazi tena kwetu".

 

 

 

Chanzo; Millard Ayo

Kuhusiana na mada hii: