Tume huru ya uchunguzi wa vurugu za Oktoba 29 nchini Tanzania, imezuia wanahabari kushiriki katika mahojiano yanayofanywa kati ya tume hiyo na waathirika wa vurugu, ikisema kuchapishwa kwa taarifa zao kunachagiza msongo wa mawazo.
Kwa mujibu wa tume hiyo, hatua hii imechukuliwa baada ya kuibuka kwa malalamiko kuwa taarifa binafsi za waathirika zinasambazwa mitandaoni bila ridhaa yao.
Chanzo; Dw