Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Wagonjwa 500 Kurejeshewa Uwezo wa Kuona Songwe

Zaidi ya wagonjwa 500 mkoani Songwe wamefanikiwa kurejeshewa uwezo wao wa kuona baada ya kupatiwa matibabu ya mtoto wa jicho kupitia kambi maalum ya siku sita.

Kambi hiyo imeandaliwa na Shirika la Kimataifa la Helen Keller kwa kushirikiana na madaktari bingwa kutoka hospitali za rufaa za Mbeya na Songwe, ambapo huduma hiyo imetolewa bure kwa wananchi waliojitokeza kwa wingi.

Mwakilishi wa TAMISEMI, Dkt. Kalidushi Kubingwa, amepongeza ushirikiano huo kati ya serikali na wadau, akisisitiza kuwa mpango huo ni mkombozi kwa Watanzania wenye changamoto za kuona.

Baada ya mafanikio hayo mkoani Songwe, huduma hiyo inatarajiwa kuhamia mkoani Tabora, huku wanufaika wakitoa shukrani kwa kurejeshewa matumaini ya kuona tena na kuendelea na shughuli zao za kila siku.

 

 

Chanzo; Mwananchi

Kuhusiana na mada hii: