Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Hamza Auawa kwa Kudhaniwa ni Mwizi

Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro limewakamata watu watano kwa tuhuma za kumuua Hamza Malingumu (20) katika eneo la Lukobe Manispaa ya Morogoro.

Polisi wamesema marehemu aliuawa baada ya kudhaniwa kuwa ni mwizi. Hata hivyo, mjomba wa marehemu, Ngwenje Mohamed, amesema kijana huyo alikuwa mgonjwa wa akili na alikuwa mgeni maeneo hayo akitokea Kilosa akidai alitoroka nyumbani majira ya saa tisa usiku bila mtu kujua alikokwenda.

"Kumbe walimwitia mwizi na watu kujitokeza na kumpiga hadi kupoteza fahamu,” amesema.

Amesema familia ilijaribu kumkimbiza hospitali, lakini alifariki dunia akiwa njiani. Polisi imesema uchunguzi zaidi wa tukio hilo unaendelea huku baadhi wakitiwa nguvuni kuhusiana na tukio hilo.

 

 

 

Chanzo; Nipashe

Kuhusiana na mada hii: