Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Shule Zahairishwa Kufunguliwa Kisa Uchaguzi Mkuu

Wizara ya Elimu na Michezo nchini Uganda imetangaza kuahirishwa kufunguliwa kwa shule na taasisi zote za elimu nchini humo hadi Jumanne, Februari 10, 2026, ikitaja sababu za Uchaguzi Mkuu nchini humo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na kusainiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Dk Kadrace Turyagyenda leo Ijumaa Januari 16, 2026 imeeleza kuwa shule zitafunguliwa Februari 10, 2026 badala ya Februari 2, kama taarifa ya Januari 6, 2026 ilivyoeleza.

“Taarifa hii inawahusu wadau wote wa elimu kwamba, kutokana na Uchaguzi Mkuu na kwa lengo la kulinda usalama wa wanafunzi wote, shule na taasisi zote za elimu nchini Uganda zitafunguliwa rasmi Jumanne, Februari 10, 2026,” imesema sehemu ya taarifa hiyo.

Uamuzi huo unahusu shule zote za serikali na binafsi, shule za kimataifa, vyuo vya kati pamoja na vyuo vikuu.

“Ili kuepusha sintofahamu, maelekezo haya yanajumuisha pia shule za kimataifa, taasisi za elimu ya juu na vyuo vikuu,” imeeleza taarifa hiyo.

Kwa mujibu wa Wizara, mabadiliko hayo yamelenga kutoa fursa ya kufanyika kwa mchakato wa uchaguzi kwa usalama na utulivu, huku yakipunguza athari zinazoweza kujitokeza katika shughuli za masomo na kulinda ustawi wa wanafunzi.

 

 

Chanzo; Mwananchi

Kuhusiana na mada hii: