Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Maelfu Waandamana Njee ya Ikulu Mexico, Gen z Watajwa

Maelfu wananchi wa Mexico wameandamana jumamosi hii Novemba 15 mpaka nje ya Ikulu ya Mexico anakoishi Rais wa nchi hiyo Claudia Sheinbaum, wakipinga uhalifu, rushwa na kutokujali kwa serikali yake.

Maandamano hayo yaliandaliwa na vikundi vya vijana vya Gen Z, wakipata uungwaji mkono kutoka kwa raia wanaopinga mauaji ya watu mashuhuri, ikiwa ni pamoja na mauaji ya wiki chache zilizopita ya Meya wa Uruapan, Carlos Manzo, ambaye alikuwa ametaka hatua kali zichukuliwe dhidi ya magenge ya uhalifu.

Maandamano hayo mengi yalikuwa ya amani lakini yalimalizika kwa baadhi ya vijana kupigana na polisi. Waandamanaji waliwashambulia polisi kwa mawe, fataki, fimbo na minyororo, kunyakua ngao za polisi na vifaa vingine.

Katibu wa usalama wa mji mkuu, Pablo Vázquez alisema watu takribani 120 walijeruhiwa, 100 kati yao ni maafisa wa polisi. Pia watu 20 walikamatwa. Rais wa Mexico, Claudia Sheinbaum alisema maandamano hayo yaliyofanyika pia katika miji mingine, yamefadhiliwa na wanasiasa wa upinzani wanaopinga serikali yake.

 

Chanzo; Tanzania Journal

Kuhusiana na mada hii: