Watu wengi wamekimbilia kuchimba dhahabu katika eneo la makazi duni mashariki mwa mji wa Johannesburg, Afrika Kusini, baada ya tangazo kutolewa siku chache zilizopita kuwa kuna dhahabu eneo hilo.
Mkaazi mmoja wa eneo hilo lililoko karibu na eneo la migodi la Springs alisema alipata chembe chembe za dhahabu akiwa analima karibu na zizi la ngombe.
Makumi ya watu sasa wamehamia eneo hilo wakichimba karibu na zizi la ngombe wakiwa na matuamaini ya kutajirika.
Wakiwa wamejihami na mapanga na majembe, wamekuwa wakichambua udongo katika eneo linalofanana na eneo la awali Afrika Kusini ilichimba dhahabu na kujitajirisha mwongo mmoja uliopita
Chanzo; Nipashe