Mahakama ya Hong Kong imemhukumu bilionea na mwanaharakati maarufu wa kuunga mkono demokrasia, Jimmy Lai, kifungo cha miaka 20 jela baada ya kupatikana na hatia ya makosa yanayohusiana na ukiukaji wa sheria ya usalama wa taifa, hatua ambayo imezua mjadala mkali ndani na nje ya China.
Lai, mwenye umri wa miaka 78 na raia mwenye pasipoti ya Uingereza, alikutwa na hatia ya njama ya kushirikiana na nguvu za kigeni pamoja na kuchapisha nyenzo zilizoelezwa kuwa zinahatarisha usalama wa taifa. Mahakama ilisema alitumia nafasi yake kama mmiliki wa gazeti la Apple Daily kuhimiza shinikizo la kimataifa dhidi ya Beijing na kuchochea upinzani wa kisiasa Hong Kong.
Chanzo; Global Publishers