Hali ya ukame imewaacha zaidi ya watu milioni 2 wakikabiliwa na njaa katika sehemu za Kenya, huku jamii za wafugaji ng'ombe kaskazini mashariki mwa nchi hiyo zikiwa zimeathiriwa zaidi, hayo ni kwa mujibu wa ripoti ya Umoja wa Mataifa.
Katika wiki za hivi karibuni, picha za mifugo iliyodhoofika katika eneo kame karibu na mpaka wake na Somalia zimewashtua wengi katika eneo hilo ambalo linaathiriwa na athari za mabadiliko ya hali ya hewa.
Athari hizo zinatajwa kuenea hadi katika nchi za Somalia, Tanzania na hata Uganda, ambapo wengi wako hatarini kutokana na hali mbaya ya hewa na uhaba wa maji, Shirika la Afya Duniani lilisema mwishoni mwa Januari.
Chanzo; Dw