Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Mwili wa Joshua Aliyeuwawa Israel Kuwasili Tanzania

Mwili wa Mtanzania Joshua Mollel, aliyeuawa na kundi la Hamas nchini Israel miaka miwili iliyopita, unatarajiwa kuwasili kesho katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) ukitokea Tel Aviv, Israel. Mollel alikuwa nchini humo akifanya mafunzo ya kilimo katika eneo la Kusini mwa Israel.

Leo, Ubalozi wa Tanzania nchini Israel uliandaa ibada maalumu ya kumuaga marehemu kabla ya safari ya kurejeshwa nchini.

Israel imekabidhi jumla ya miili 285 ya Wapalestina kwa upande wa Palestina, ikiwa ni sehemu ya makubaliano yaliyowezesha kupokelewa kwa miili ya mateka 19 Waisraeli waliorejeshwa na Hamas, pamoja na miili ya mateka watatu raia wa kigeni,raia mmoja wa Thailand, mmoja wa Nepal na Mtanzania mmoja.

 

Chanzo; Bbc

Kuhusiana na mada hii: