Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Marekani Waionya Uingereza Kisa Palestina

Wanasiasa wa Marekani wameionya Uingereza na washirika wake wengine dhidi ya kuitambua Palestina kama dola huru, wakisema hatua hiyo itawapa nguvu wanamgambo wa Hamas na kutishia usalama wa Israel.

Wanasiasa hao wa chama cha Republican akiwemo mbunge wa New York Elise Stefanik na Seneta Rick Scott, wameyatumia barua mataifa ya Uingereza, Ufaransa, Canada na Ausrealia pamoja na washirika wengine muhimu, wakiwataka kupinga juhudi katika mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa za kuihalalisha na kuitambua Palestina kama dola huru.

Waziri Mkuu wa Uingereza Keir Starmer anatarajiwa kutangaza rasmi uamuzi wa nchi yake kuitambua Palestina kesho Jumapili

 

Chanzo; Dw

Kuhusiana na mada hii: