Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Cameroon Serikali Yapewa Masaa 48 Kuachia Wafungwa

Yaoundé, Cameroon – Issa Tchiroma Bakary, mgombea wa upinzani ambaye pia amejitangaza mshindi wa uchaguzi wa rais, amempa Rais Paul Biya na serikali yake masaa 48 kuachilia huru watu wote waliokamatwa baada ya uchaguzi wa Oktoba 12.

Tchiroma ametoa onyo hilo huku akipinga rasmi matokeo ya uchaguzi, akisema Wakameruni watalazimika kuchukua hatua wenyewe iwapo wafungwa hao hawataachiliwa. Hii inajiri baada ya kipindi cha ukimya wake usio wa kawaida kwa siku kadhaa.

Ripoti za Umoja wa Mataifa zinaonyesha kuwa watu 48 wamepoteza maisha katika ghasia za baada ya uchaguzi, huku Tume ya Kitaifa ya Haki za Binadamu ikiripoti kuwa zaidi ya watu 1,200 wamekamatwa.

 

Chanzo; Global Publishers

Kuhusiana na mada hii: