Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Taliban Vitabu Vilivyoandikwa na Wanawake Vyaondolewa

Serikali ya Taliban imeondoa vitabu vilivyoandikwa na wanawake katika mfumo wa kufundisha wa vyuo vikuu nchini Afghanistan kama sehemu ya marufuku mpya ambayo pia imeharamisha ufundishaji wa haki za binadamu na unyanyasaji wa kijinsia.

 

Baadhi ya vitabu 140 vya wanawake - ikiwa ni pamoja na "Safety in the Chemical Laboratory" - vilikuwa miongoni mwa vitabu 680 vilivyopatikana kuwa "visivyo sahihi" kutokana na "sera za kupinga Sharia na Taliban".

Vyuo vikuu vilielezwa kuwa haviruhusiwi tena kufundisha masomo 18, huku afisa wa Taliban akisema "vinakinzana na kanuni za Sharia na sera ya mfumo".

 

Amri hiyo ni ya hivi punde zaidi katika mfululizo wa vikwazo ambavyo Taliban wameviweka tangu warudi madarakani miaka minne iliyopita.

 

Chanzo: Bbc 

Kuhusiana na mada hii: