Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Tishio, Trump Kushambulia Nigeria

Rais Donald Trump ameonya kuwa Marekani inaweza kufanya mashambulizi mengine ya anga nchini Nigeria ikiwa mauaji ya Wakristo yataendelea.

Katika mahojiano na gazeti la New York Times, lililochapishwa siku ya Alhamisi, Trump aliulizwa ikiwa mashambulizi ya hivi majuzi ya anga ya Marekani katika jimbo la Sokoto nchini Nigeria yakilenga wanamgambo wenye itikadi kali yalikuwa sehemu ya operesheni kubwa zaidi ya kijeshi.

Akijibu swali hilo, Trump alisema: “Ningependelea liwe shambulio la mara moja.” Hata hivyo, aliongeza kwa msisitizo: “Iwapo mauaji dhidi ya Wakristo yataendelea, basi yatakuwa mashambulizi ya mara kwa mara.”

Utawala wa Trump hapo awali umeikosoa vikali Serikali ya Nigeria kwa kile ilichokitaja kuwa kushindwa kuwalinda Wakristo dhidi ya mashambulizi ya wanamgambo wa jihadi.

 

 

Chanzo; Itv

Kuhusiana na mada hii: