Rais wa Sudan Kusini, Salva Kiir, amemteua bila kukusudia Steward Sorobia Budia, aliyefariki dunia, kuwa mjumbe wa kamati itakayohusika na maandalizi ya uchaguzi wa nchi hiyo.
Kwa mujibu wa msemaji wa Ofisi ya Rais, makosa yalitokea katika mchakato wa uteuzi baada ya jina la Budia, mwanasiasa wa zamani wa upinzani, kujumuishwa miongoni mwa wajumbe waliotajwa katika amri ya rais.
Taarifa zinaeleza kuwa Budia alifariki dunia takribani miaka mitano iliyopita.
Aidha, familia ya marehemu imeripotiwa kudai fidia, ikieleza kuwa kwa mujibu wa tamaduni zao, hairuhusiwi kumtaja au kuamsha roho ya marehemu bila ridhaa au ushiriki wa familia.
Chanzo; Crown Media