Waziri Mkuu wa Nepal, KP Sharma Oli, amejiuzulu kufuatia hasira kali ya umma baada ya vifo vya watu 22 waliouawa kwenye makubaliano kati ya polisi na waandamanaji waliokuwa wakipinga ufisadi.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka ofisi yake, kujiuzulu kwake kumelenga kufungua njia ya kupatikana kwa suluhisho la kikatiba kufuatia maandamano makubwa yanayoongozwa na vijana, yaliyosababishwa na tuhuma za ufisadi uliokithiri na marufuku ya mitandao ya kijamii ambayo sasa yameondolewa.
Maandamano hayo yaligeuka kuwa ya vurugu siku ya Jumatatu, baada ya maelfu ya waandamanaji wengi wao wakiwa wamebeba mabango yaliyokuwa na maandishi kuwa ni vijana wa kizazi cha Gen Z, Waliingia barabarani jijini Kathmandu.
Inakadiriwa kuwa watu takriban 200 walijeruhiwa katika makabiliano hayo, ambapo polisi walitumia gesi ya kutoa machozi, magari ya maji ya kuwatawanya waandamanaji, na hata risasi za moto.
Siku ya Jumanne, maandamano yaliendelea kwa kasi, huku waandamanaji wakichoma moto jengo la bunge, makao makuu ya Chama cha Congress cha Nepal, na nyumba ya aliyewahi kuwa Waziri Mkuu, Sher Bahadur Deuba.
Zaidi, Nyumba za viongozi wengine wa kisiasa pia zilivamiwa na kuharibiwa.
Chanzo: Bbc Swahili