Kwa mara ya kwanza Rwanda imekiri kuwa inashirikiana na kundi la waasi wa AFC/M23 katika vita vinavyoendelea mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Balozi wa Rwanda nchini Marekani Mathilde Mukantabana ameiambia kamati ya Bunge nchini Marekani kuwa Rwanda inafanya hivyo ili kulinda maslahi ya raia wa Kongo wanaozungumza kinyarwanda lakini pia kuzuia uwezekano wa kutokea mauaji mengine kama yale yaliyotokea Rwanda mwaka 1994.
Chanzo; Dw