Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Jeshi Letu Halipigi Wanawake, Uganda

Mkuu wa Jeshi la Uganda, Jenerali Muhoozi Kainerugaba, amesema jeshi la Uganda halipigi wanawake kama kiongozi wa upinzani, Robert Kyagulanyi, maarufu Bobi Wine anavyodai.

Jenerali Kainerugaba ambaye pia ni mtoto wa Rais Yoweri Museveni, amebainisha hayo akijibu tuhuma za wanajeshi wake kuvamia nyumbani kwa Bobi Wine na kuwatesa watu na kumpiga mke wake.

“Jeshi letu haliwapigi wanawake,” ameandika Kainerugaba.

Bobi Wine alidai kwamba askari walivamia makazi yake usiku katika kitongoji cha Magere jijini Kampala, waliwadhalilisha baadhi ya wafanyakazi na kumkaba mke wake.

Kiongozi huyo amesema hakuwepo nyumbani wakati wa tukio hilo kwani tangu uchaguzi wa urais ulioibua utata nchini humo ameendelea kuishi mafichoni ili kuepuka kushikiliwa.

 

 

Chanzo; Mwananchi

Kuhusiana na mada hii: