Imebainika kwamba rais wa Syria Ahmad al Sharaa na mawaziri wake wa ndani na nje walinusurika kuuawa mara tano kwenye njama dhidi yao mwaka uliopita, kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa na Umoja wa Mataifa juu ya kitisho cha kundi lijiitalo Dola la Kiislamu, IS, ripoti iliyotolewa wakati Marekani ikiondosha vikosi vyake Syria vilivyodaiwa kuwako huku kupambana na kundi hilo.
Ripoti hiyo, iliyotolewa Jumatano na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres, inaangazia kwa kina mazingira ya kiusalama nchini Syria na juhudi za makundi ya kigaidi kudhoofisha serikali mpya ya nchi hiyo.
Chanzo; Dw