Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu akiweka stika nyekundu ya usalama juu ya kamera ya nyuma ya simu yake akiwa karibu na jengo la Knesset (Jengo la Bunge lipo mjini Jerusalem)
Hatua hiyo inaonekana kama tahadhari dhidi ya programu hatari za ujasusi (spyware) ambazo zinaweza kuwasha kamera ya simu bila mtumiaji kujua.
Katika maeneo nyeti ya kiusalama hata viongozi wakuu hutumia njia rahisi kama kufunika kamera kwa stika au kifuniko maalum ili kupunguza hatari ya udukuzi na ufuatiliaji wa kijasusi.
Wataalamu wa usalama wa mtandao wanasema kuwa mbinu hiyo rahisi bado ni mojawapo ya njia bora za kuzuia upatikanaji wa matukio kwa njia isiyoidhinishwa.
Chanzo; Bongo 5