Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Changamoto Zilizoandama Utawala wa Maduro, Venezuela

Rais wa Venezuela, Nicolàs Maduro yupo jijini New York, Marekani anakoshikiliwa baada ya kutekwa na Vikosi vya Marekani ambapo leo Jumatatu, anatarajiwa kupandishwa mahakamani na kusomewa mashtaka yanayomkabili.

Utawala wa Maduro nchini Venezuela, ulitawaliwa na changamoto nyingi kati yake na wapinzani, wakosoaji, wanaharakati na raia wa kawaida.

Miongoni mwa mambo ambayo Maduro alikuwa akilalamikiwa sana, ni pamoja na kudorora kwa kiasi kikubwa kwa uchumi licha ya nchi hiyo kuwa na utajiri wa rasilimali na ukandamizwaji wa demokrasia, kusakamwa kwa wapinzani na kufanyika kwa chaguzi zisizokuwa za haki.

Mfumuko wa bei, upungufu mkubwa wa bidhaa muhimu kama chakula, dawa na mahitaji mengine ya kibinadamu vikachangia wananchi maskini wa Venezuela kuendelea kula msoto mkali kila kukicha.

 

 

Chanzo; Global Publishers

Kuhusiana na mada hii: