Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Waziri Roboti “AI” Ateuliwa Albania

Tirana, Albania imerekodi rekodi ya dunia kwa kuwa nchi ya kwanza kuteua waziri aliyeundwa kwa akili bandia (AI), siyo waziri wa teknolojia ya AI, bali waziri halisi wa kidijitali, aliyeundwa kwa misimbo na kuendeshwa na mfumo wa kisasa wa akili bandia.

Jina lake ni Dieella, linalomaanisha 'mwanga wa juu' kwa Kialbania ndilo jina la roboti, atasimamia shughuli zote za manunuzi ya umma, kama alivyoeleza Waziri Mkuu Edi Rama.

Aliteuliwa rasmi Alhamisi ya Septemba 11, 2025, ambapo Rama alimtambulisha kama"mwanachama wa baraza la mawaziri asiye na uwepo wa kimwili," ambaye atahakikisha kuwa zabuni za umma zitakuwa huru kwa asilimia 100 dhidi ya ufisadi.

 

Chanzo: Mwananchi

Kuhusiana na mada hii: