Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Gen Z, Watajwa Kushuka kwa Sekta ya Pombe Duniani

Kwa mujibu wa tafti mpya zinaonyesha sekta ya pombe duniani imepoteza takriban $830 bilioni katika miaka minne iliyopita, huku kizazi cha Gen Z kikitajwa kuongoza mabadiliko ya mtazamo kuhusu unywaji.

Wengi wa kizazi hicho wameamua kunywa kwa uangalifu zaidi, kupunguza au kuacha kabisa, wakipa kipaumbele afya ya akili, ustawi, na maisha bila pombe. Hali hiyo imesababisha kushuka kwa mauzo ya bia, divai na pombe kali, na kuongezeka kwa umaarufu wa mocktails, vinywaji visivyo na kilevi na vyenye kiwango kidogo cha pombe.

Kampuni kubwa za pombe sasa zimeanza kuwekeza kwenye bidhaa zisizo na kilevi, wakikiri kuwa huu si mtindo wa muda mfupi bali ni mabadiliko ya kijamii yanayoathiri tasnia nzima.

 

 

Chanzo; Nipashe

Kuhusiana na mada hii: