Polisi wa Uganda wamewakamata wanawake wawili, wote wakiwa katika umri wa miaka 20, baada ya majirani kuripoti kuwaona wakibusiana hadharani, kitendo ambacho kimeharamishwa chini ya Sheria ya Kupinga Mapenzi ya Jinsia Moja nchini humo.
Katika taarifa iliyotolewa jana na Jeshi la Polisi nchini humo, walisema wawili hao walikamatwa huko Arua, kaskazini magharibi mwa Uganda, na kwamba majirani waliwapiga picha kabla ya kuwaarifu polisi.
Pia ilielezwa kuwa wanawake hao wanaendelea kuzuiliwa bila kupata uwakilishi wa kisheria.
Sheria ya nchi hiyo inatoa adhabu kali, ikiwa ni pamoja na kifungo cha maisha jela na hukumu ya kifo kwa mahusiano ya jinsia moja, na kwamba adhabu hizo ziliwekwa kwasababu idadi ya kesi za aina hiyo zimezidi kiwango.
Polisi waliarifiwa na majirani waliosema wawili hao walikuwa wamejihusisha na tabia ya mapenzi ya jinsia moja, AFP inaripoti.
Chanzo; Nipashe