Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Netanyahu Akatiza Anga za Nchi Ziitambuazo ICC Licha ya Hati ya Kukamatwa

Ndege iliyombeba Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, kuelekea Florida, Marekani, kwa mkutano na Rais wa Marekani Donald Trump, imepita katika anga za Ugiriki, Italia na Ufaransa nchi wanachama wa Mkataba wa Roma unaotambua Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC).

Kwa mujibu wa takwimu za FlightRadar, ndege hiyo iliingia Bahari ya Atlantiki baada ya kupita anga za mataifa hayo, licha ya kuwepo kwa hati ya kukamatwa dhidi ya Netanyahu iliyotolewa na ICC.

Safari hiyo ilifuata njia tofauti na ile aliyotumia Netanyahu mwezi Septemba mwaka huu alipokwenda New York kuhudhuria Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, ambapo alitumia anga za Ugiriki na Italia pekee bila kuingia anga ya Ufaransa.

Hatua hiyo imeibua maswali mapya kuhusu utekelezaji wa wajibu wa nchi wanachama wa ICC na msimamo wao wa kisiasa katika kesi zinazohusu uhalifu wa kivita.

 

 

Chanzo; Cnn

Kuhusiana na mada hii: