Raia wa Uganda Vicky Ajok aliyekuwa akifanya kazi za ndani huko nchini Syria amehukumiwa kifo baada ya kukutwa na hatia ya kumuua aliyekuwa muajiri wake raia wa Syria.
Wakati hukumu hiyo ikitarajiwa kutekelezwa Februari 28, mwaka huu, Shirika la Migrant Workers Voice Uganda limewahimiza maofisa jijini Kampala kuzungumza na wenzao wa Syria ili kusimamisha utekelezaji wa hukumu hiyo dhidi ya Vicky.
Imeelezwa kuwa Vicky alihukumiwa kwa kumuua mwajiri wake mwenye umri wa miaka 87, Huda Shaarawi, ambaye ni mwigizaji maarufu wa tamthilia za televisheni nchini Syria.
Tukio hilo lilitokea mwezi uliopita katika mji mkuu wa Syria, Damascus.
Chanzo; Nipashe