Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Martin Apigwa Risasi Eneo la Makazi ya Trump

Mwanaume mwenye silaha ameuawa kwa kupigwa risasi baada ya kukaribia eneo la makazi ya Rais wa Marekani Donald Trump huko Florida, imethibisha Idara ya Usalama wa Rais.

Mwanaume huyo alikuwa amebeba bunduki na kopo la mafuta aliposimamishwa kabla ya kupigwa risasi na maafisa wa Usalama.

Tukio hilo lilitokea jana Jumapili asubuhi, wakati Rais alipokuwa Washington DC. Mshukiwa ametajwa kama Austin T Martin kutoka Cameron, North Carolina.

Familia yake huko North Carolina imeripoti kupotea kwake mapema Jumapili asubuhi, Ofisi ya Polisi eneo la Moore imethibitisha hilo.

Ofisi ya Usalama imesema haina historia yoyote ya uhalifu inayomhusu Martin, lakini alipigwa risasi baada ya kukataa amri.

 

 

Chanzo; Itv

Kuhusiana na mada hii: