Rais Donald Trump amekanusha taarifa kwamba mkuu wa majeshi ya Marekani, Jenerali Dan Caine, aliwahi kuonya juu ya hatari za operesheni dhidi ya Iran. Trump amesema ripoti hizo “si za kweli” na kudai kuwa Marekani “ingeishinda Iran kwa urahisi” endapo vita vingalizuka.
Vyombo vya habari vya Marekani vimemnukuu Caine akionya kuhusu hatari za mzozo wa muda mrefu, upungufu wa silaha na uwezekano wa vikosi vya Marekani kukumbwa na vifo endapo mashambulizi yangelifanyika.
Trump amesema bado anapendelea diplomasia, lakini akatahadharisha kwamba kukosekana kwa makubaliano “kutakuwa siku mbaya sana” kwa Iran.
Chanzo; Dw