Rais wa Marekani Donald Trump amesema kuwa yeye na mwenzake wa China Xi Jinping wamefikia makubaliano kuhusu mustakabali wa mtandao wa kijamii wa TikTok nchini Marekani walipozungumza kwa njia ya simu siku ya Ijumaa, ingawa Beijing haijathibitisha hilo.
Trump aliandika kwenye Mtandao wake wa Truth Social kwamba mazungumzo yetu yalikuwa “na tija” na kwamba “alithamini” hatua ya Xi ya kuidhinisha makubaliano hayo, ambayo yataiwezesha TikTok nchini Marekani kununuliwa na kundi la wawekezaji wa Marekani.
Shirika rasmi la habari la serikali ya China Xinhua halikuangazia kikamilifu matokeo ya mazungumzo hayo, huku Xi akinukuliwa akisema kuwa Beijing “inakaribisha mazungumzo kuhusu TikTok”.
TikTok, ambayo inaendeshwa na kampuni ya Kichina ya ByteDance, hapo awali ilishauriwa kuuza biashara yake kwa Wamarekani la sivyo itakabiliwa na tishio la kufungwa.
Chanzo: Bongo 5