Duru ya pili ya mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja kati ya Iran na Marekani imefanyika mjini Geneva chini ya usimamizi wa Oman.
Muda mfupi kabla ya mazungumzo hayo, kiongozi mkuu wa Iran, Ayatollah Ali Khamenei, alitoa onyo kwa Rais Donald Trump, akisisitiza kwamba Marekani "haiwezi kuiangusha Jamhuri ya Kiislamu."
Kauli ya Khamenei ameitoa kwenye hotuba yake kwa taifa hii leo siku chache baada ya Trump kusema mabadiliko ya kiutawala ni kitu muhimu kinachopaswa kufanyika Iran.
Chanzo; Dw