Search

Saved articles

You have not yet added any article to your bookmarks!

Browse articles

GDPR Compliance

We use cookies to ensure you get the best experience on our website. By continuing to use our site, you accept our use of cookies, Privacy Policy, and Terms of Service.

Jeshi la Mapinduzi la Iran la Orodheshwa Makundi ya Kigaidi

Mawaziri wa mambo ya nje wa Umoja wa Ulaya wamekubaliana kulitangaza jeshi la Walinzi wa Mapinduzi la Iran (IRGC) kuwa ni kundi la kigaidi. Akizungumza mjini Brussels wakati wa mkutano wa mawaziri wa mambo ya nje wa EU, Mkuu wa sera za kigeni wa umoja huo Kaja Kallas amesema “utawala wowote unaowaua maelfu ya watu wake unajiangamiza wenyewe.”

Msimamo huo wa pamoja unaanzisha utaratibu wa kisheria wa kurasimisha tamko hilo ambalo linachukuliwa kuwa la ishara kubwa kwa sababu jeshi hilo tayari limewekewa vikwazo na EU kwa ukiukaji wa haki za binadamu.

Huku baadhi ya mawaziri wa EU wakidokeza kwamba hadi watu 30,000 huenda waliuawa katika ukandamizaji mkali dhidi ya maandamano ambayo yameikumba Iran, shinikizo limeongezeka kwa Umoja wa Ulaya kuchukua uamuzi huo.

 

 

 

Chanzo; Dw

Kuhusiana na mada hii: